23 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

JWTZ laonya watakaovuruga amani

Editha Karlo,Kigoma

JESHI la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limesema litawaadhibu wale wote watakaojaribu kuvuruga amani na usalama wa nchi.

Jeshi hilo, limetoa tahadhari kwa watu wanaotumia mapori ya akiba vibaya kuacha kufanya hivyo.

Kauli hiyo, imetolewa na Mkuu wa Brigedi ya Kanda ya Magharibi (202 Kikundi cha Vikosi), Brigedia Jenerali Julius Mkunda jana, wakati wakati akiahirisha zoezi la kijeshi la kujiweka tayari kwa wapiganaji kupambana na adui.

“Amani na usalama wa Watanzania, lazima upewe kiupaumbele, yeyote atakayejaribu kuchezea amani tutamshughulikia,”alisema.

Zoezi hilo ambalo lilifanyika kwenye mapori ya wilaya za Kibondo, Kasulu na Kakonko na kupewa jina la Opereshini KIKAKA, lilikuwa la mafanikio makubwa.

Brigedia Jenerali Mkunda alisema kumekuwa na uharibifu mkubwa wa mapori kutumika kwa shughuli za maficho ya ujambazi, uwindaji haramu na kilimo mambo ambayo yanafanywa na wageni kutoka nchi jirani.

“Tanzania sio shamba la bibi kwa kila anayetaka anakuja kufanya anachojisikia, hatutakubali tutawaadhibu wote wenye nia mbaya ya kutumia mapori yetu kwa vitendo ambavyo ni kinyume cha sheria na taratibu za nchi yetu, vinatishia amani na usalama wa raia na mali zao na kuwafanya waishi kwa  woga,”alisema Brigedia Jenerali Mkunda.

 Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Mkuu wa Mafunzo na Utendaji Kivita kutoka Brigedi ya Kanda ya Magharibi, Kanali Wilbert Ibuge alisema mapori yote ambayo watu wanayaona nchini yana wenyewe na wenyewe ni jeshi hilo ambalo lina wajibu wa kuyatunza.

“Tuna wajibu wa kuyatunza mapori haya, hakuna mtu yeyote ambaye ataingia akaachwa ayatumie anavyotaka,”alisema.

Alisema mafunzo hayo, ni sehemu ya utimamu na utayari wa jeshi kujindaa kupambana pindi adui anapotokea na kwa sababu kwenye vita hakuna mahali pa kufanya majaribio.

Alisema kazi ya kuwasaka na kuwakamata wote ambao wataingia kwenye mapori hayo na kufanya vitendo vya uhalifu, itatumika kama sehemu ya mazoezi kwa vitendo kwa wapiganaji.

 Mkuu wa Kikosi cha 24, ambacho kimesimamia na kuratibu mafunzo hayo, Meja J.S.Luhonyva alisema  mazoezi hayo yamefanikiwa kwa kiasi kikubwa na vijana wameonyesha tayari kukabiliana na adui.

Alisema lengo la mazoezi hayo kwa kiasi kikubwa limefikiwa medani zote za mapambano ya kivita. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Kigoma,Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga, Mkuu wa Wilaya Kasulu, Kanali Simon Hanange alisema mazoezi hayo yatasaidia mkoa kuendelea kuwa na aman muda wote.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles