31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Juni Mosi mwisho wa matumizi ya mifuko ya plastiki

Brighiter Masaki

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba amesema kuanzia Juni Mosi mwaka huu itakuwa ndio mwisho wa matumizi ya mifuko ya plastiki na Sheria kali zitachukuliwa kwa yeyote atakayekiuka maagizo hayo.

Amesema hayo Mei 22 Jijini Dar es Salaam, kwenye kikao cha viongozi na watendaji mkoani hapo kilichokuwa kinahusu marufuku ya matumizi ya mifuko ya plastiki.

Makamba Amesema, ofisi yake kwa kushirikiana na ofisi ya Tamisemi watapita kwenye maduka na Magenge kwa ajili ya kukagua na kuangalia kama agizo linatekelezwa.

“Wazalishaji wa mifuko hiyo wakibainishwa bado wanazalisha faini itakuwa shilingi milioni 20 na kifungo, waingizaji katoka nje nao faini milioni 20, huku mtumiaji faini yake ikiwa ni 30,000.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles