27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

JOH MAKINI, DOGO JANJA KUPAMBA KILI MARATHON 2017

NA MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM


WASANII wa muziki wa kizazi kipya, Joh Makini na Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’, wanatarajiwa kutoa burudani katika mbio za Kilimanjaro Marathon 2017, Jumapili hii mjini Moshi.

Akizungumza jijini Moshi jana, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Pamela Kikuli, aliwataka wakazi mkoani hapa kujitokeza kwa wingi katika mbio hizo ambazo ni kubwa Tanzania.

“Wasanii hawa wanakubalika Moshi, tuna uhakika mashabiki watajitokeza kwa wingi kuangalia mbio na kupata burudani,” alisema Pamela.

Upande wake Joh Makini alisema amejiandaa vizuri kukonga nyoyo za mashabiki wake na kuwataka wakazi wa Moshi kujitokeza kwa wingi kushuhudia burudani iliyoandaliwa.

Naye Dogo Janja alisema anafarijika kupata nafasi hiyo, kwani mkoa huo ni miongoni mwa mikoa yenye mwamko mkubwa wa mashabiki.

Usajili mjini Moshi ulianza kufanyika jana, huku wakazi mbalimbali wakiwa wamejitokeza kujiandikisha kushiriki mbio hizo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles