26.1 C
Dar es Salaam
Saturday, March 30, 2024

Contact us: [email protected]

JKT watakiwa kukamilisha mradi wa hospitali Kimara

Na Brighiter Masaki, Dar es Salaam

Katibu Mkuu Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), Elirehema Moses Kaaya, amewataka Jeshi la Polisi (JKT) kukamilisha mradi wa Hospital iliyopo Kimara Baruti kwa haraka ili wananchi wawezekupata matibabu.

Akizungumza na www.mtazania.co.tz mapema leo wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi ya maendeleo ya Manispaa ya Ubungo, Kaaya amewataka JKT kukamilisha mradi kwa wakati ili ianze kutoa huduma.

“Wananchi wa Kimara Baruti wanahitaji huduma ya matibabu ya haraka hivyo niwaombe, JKT kufanyakazi usiku na mchana ili kuweza kukamirisha mradi wa hospital kwa wakati.

“Lengo ni wanachi wapate huduma ya matibabu kwa haraka kwasababu walizoea kwenda mbali kupata matibabu lakini kwasasa utakapo kamilika watapata huduma zote,” amesema Kaaya

Kwa upande wake mkazi wa Kimara Baruti, Happiness Kileo, amesema kuwa mradi unaendelea vizuri na wanaipongeza serikali kwa maendeleo wanayowapelekea wananchi hasa ya matibabu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles