23.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

JINSI YA KUPIKA CHAPATI ZA MAZIWA

MAHITAJI

Maziwa ½ lita

Ngano 1 kilo

Mafuta

Chumvi kijiko kimoja cha chakula

 

JINSI YA KUPIKA

Bandika mafuta kiasi jikoni yaache yachemke halafu yamimine kwenye ngano, kisha koroga na mwiko au kijiko ili usiungue mikono.

Bandika maziwa jikoni na hakikisha yamechemka vizuri kisha yamimine kwenye ngano uanze kukanda unga wako taratibu.

Wakati ukikanda ongeza maziwa kama mchanganyiko wako bado mzito na endelea kufanya hivyo hadi uwe mwepesi.
Unga ukiwa tayari kata matonge halafu anza kusukuma chapatti kwa ajili ya kuchoma.

Wakati unachoma acha iive mpaka upate rangi ya kahawia, geuza upande wa pili na kuongeza mafuta kidogo huku ukiendelea kuigeuza geuza mpaka iive.

Baada ya kuiva ondoa na kuweka kwenye sahani safi na hadi hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Chakula hiki kinaweza kuliwa asubuhi kama kifungua kinywa au jioni sambamba na mchuzi wa nyama, maharagwe au supu ya samaki.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles