27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

JINA LAMTESA AUNTY EZEKIEL

Na KYALAA SEHEYE


STAA wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel, ameweka wazi kwamba kipindi cha mfungo wa Ramadhan kinapofika kila mwaka hujikuta akiona aibu kula hadharani, kutokana na jina lake la Rahma alilolitumia kipindi alipobadili dini.

Aunty aliwahi kubadili dini wakati alipoolewa na Sunday Demonte, anayetumikia kifungo cha miaka kumi jela huko Abu Dhabi.

“Mimi ni Mkristo, ila Rahma ni jina ambalo nililipenda na mara ifikapo mwezi huu basi najikuta nakuwa Rahma zaidi kuliko Aunty, kwa kuwa jina hili nililipenda tangu utotoni na hata nilipobadili dini nilipenda kulitumia, lakini naona linanitesa zaidi ikifika mwezi huu wa Ramadhan, maana najikuta nashindwa kula au kunywa mchana kwa sababu ya jina hili,” alisema Aunty Ezekiel.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles