30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

JICA yatoa Sh bil 116 za maendeleo

JICA-02Na Asifiwe George, Dar es Salaam

SHIRIKA la Maendeleo la Japan (JICA) na Wizara ya Fedha na Mipango, wamesaini mkataba wa mkopo wa Sh bilion 116 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Mwakilishi Mkuu  wa Ofisi ya JICA Tanzania,Toshio Nagase, alisema mradi huo utahusisha mfululizo wa mageuzi ya sera za maendeleo ambao utaondoa vikwazo katika mazingira muhimu ya biashara, hasa sekta ya viwanda na kutoa ajira.

Alisema mradi huo, utashughulikia maeneo makuu yenye vikwazo kwa lengo la kurahisisha usajili wa biashara na upatikanaji wa leseni ili kupata ufanisi na umahiri wa utawala wa forodha hasa katika bandari.

“Shirika limedhamiria kuunga mkono Serikali mpya  katika njia mbalimbali ili kuharakisha juhudi za kuifanya Tanzania iwe nchi ya viwanda na uchumi wa kati kama ilivyoainishwa katika Dira ya Mandeleo ya mwaka 2025 , “alisema.

Naye Ofisa Habari wa JICA, Helen Masele alisema mkopo huo pia utasaidia kuboresha ufanisi wa ulipaji na urekebishaji motisha ya kodi.

Wakati huo huo, shirika hilo limekubali kufanya utafiti wa awali wa mradi wa uboreshaji wa miundombinu  ya usambazaji wa maji visiwani Zanzibar.

Alisema madhumuni ya utafiti huo, ni kufanya upembuzi yakinifu wa mradi kitaalamu kwa lengo la kuboresha mazingira ya kuishi  kwa watu wa Zanzibar.

“JICA imekuwa ikisaidia miradi miwili  ya sekta ya maji tangu mwaka  2005/2010, ambapo zaidi ya Sh bilioni 50 zilijenga visima vikubwa, hifadhi za maji, mabomba ya maji na vifaa vya usambazaji wa maji,” alisema Masele.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles