27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

JELA MIAKA 60 KWA KUKUTWA NA MGUU WA TWIGA

 

Na GURIAN ADOLF-SUMBAWANGA

MAHAKAMA ya Wilaya ya Mlele mkoani Katavi, imewahukumu kifungo cha jumla ya miaka 60 jela washtakiwa watatu waliotiwa hatiani kwa kukutwa na mguu wa twiga kinyume cha sheria za wanyama pori.

Hukumu hiyo imetolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Teotimus Swai, baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka.

Awali, mwendesha mashtaka Wakili wa Serikali, Jamila Miraji, alisema mahakamani hapo kuwa washtakiwa hao kwa pamoja walikamatwa Oktoba 11, mwaka jana saa 5:30 wakiwa na mguu wa twiga kinyume cha sheria za wanyama pori.

Aliieleza mahakama hiyo kwamba washtakiwa walikamatwa na askari wa Tanapa waliokuwa katika doria ndani ya hifadhi ya wanyamapori ya Katavi, ambako waliwakuta na mguu huo wa twiga.

Akitoa hukumu hiyo, hakimu Swai alisema ushahidi uliotolewa mahakamani na upande mashtaka umewatia hatiani watuhumiwa hao.

Kabla ya hukumu hiyo, hakimu Swai alitoa nafasi ya kujitetea kwa watuhumiwa, ambao waliiomba mahakama isitoe adhabu kali kwao kwa kuwa ni wategemezi, maombi ambayo yalitupiliwa mbali.

Waliohukumiwa kwenda jela ni Juma Kinanda (66), Saidi Shabani (42) wote wakazi wa Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora na Rashidi Miraji (64) mkazi wa Inyonga wilayani Mlele.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles