30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

JB Maeba atimiza ndoto zake na Cannibal

NA CHRISTOPHER MSEKENA

MSANII wa Afro Pop na Bongo Fleva anayeishi Kenya, James Tesha a.k.a JB Maeba, amesema anafurahi kutimiza ndoto za kufanya wimbo, Tena na Tena na rapa nyota nchini humo, Cannibal.

Maeba ambaye ni Mtanzania anayeishi Kenya, ameliambia ukurasa huu kuwa Cannibal ni miongoni mwa wasanii wakubwa Kenya waliomvutia hivyo kufanya naye wimbo ni jambo kubwa.

“Mimi nafanya Afro Pop na Bongo Fleva yenye vionjo vya RnB. Cannibal nimekuwa nikipenda muziki wake niliporudi Tanzania huo Kenya meneja wangu alituunganisha na tukafanya kazi hii ambayo imetoka jana na inapatikana kwenye chaneli yangu ya YouTube,” alisema JB Maeba.

Aliongeza kwa kusema: “Nilianza safari yangu mnamo 2015, niliamini ninaweza kusukuma sanaa yangu ya muziki mbele zaidi, imekuwa safari ngumu ila sasa mambo yanakwenda poa kwahiyo naomba sapoti kwa mashabiki.”

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles