Pietermaritzburg, Afrika Kusini
Aliyekuwa Rais wa zamani nchini Afrika Kusini, Jacob Zuma, leo Mei 26, 2021 amesimama kizimbani na kukana mashitaka 18 yanayomkabili dhidi yake.
Katika kesi yake ya msingi iliyosikilizwa Mahakamani jijini Pietermaritzburg, mwanasiasa huyo anakabiliwa na tuhuma za rushwa, ukwepaji kodi na utakatishaji fedha.
Akizungumza kwa upole rais Jacob Zuma mwenye umri wa miaka 79, huku watu wanaomuunga mkono wakiwa wamekusanyika nje ya mahakama, amesema kesi zake ni matokeo ya siasa chafu dhidi yake.
Akifafanua hilo, Zuma hakuwataja majina lakini alisema maadui zake wanatoka ndani na nje ya Chama tawala nchini humo, African National Congress (ANC).