RAPA, Jeffrey Atkins ‘Ja Rule’, amedai kuachana na muziki baada ya albamu yake mpya anayotarajia kuiachia wakati wowote ndani ya mwaka huu.
Msanii huyo alisema licha ya muziki kumpa jina kubwa atapumzika kwa kuwa ni muda sahihi kwake kufanya mambo mengine yatakayomwongezea kipato tofauti na muziki.
“Nimefanya muziki kwa kipindi kirefu, natarajia kuachana nao baada ya kuachia albamu yangu mpya mwaka huu, nitaendelea kuupenda muziki lakini kwa sasa ni bora niwapishe wasanii wengine wauendeleze.
“Kuna mambo mengi nitayafanya likiwemo filamu, nimekuwa nikifanya filamu mbalimbali na ninaamini ninaweza kuendelea kwa muda mrefu ila sio muziki,’’ alisema Jarule.
Hata hivyo, aliongeza kwamba atakapoachana na muziki na kuingia katika filamu hataacha kujishughulisha na biashara zake mbalimbali kwa ajili ya kujipatia kipato zaidi.