ONTARIO, CANADA
BAADA ya kufanya vizuri na wimbo Imani, msanii wa kizazi kipya kutoka Ontario, Canada, Michael Baiye maarufu kama J Bwai, ametamba kuja kutikisa chati za muziki na ngoma mpya, Busy Body.
J Bwai mwenye asili ya Cameroon, ameliambia MTANZANIA kuwa muda wowote kutoka sasa ataachia audio na video ya wimbo, Busy Body wenye mahadhi ya kuchezeka.
“Nashukuru Imani ilifanya vizuri sasa muda wowote kutoka sasa naachia ngoma mpya inayoitwa Busy Body, huu ni wimbo wa klabu ambao umelenga zaidi kuwapa rapa mashabiki zangu popote walipo, kwahiyo watu waendelee ku-subscribe chaneli yangu ya YouTube, Disemba 2, mwaka huu watafurahi” alisema J Bwai.