27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

ITA: Tutaendelea kuwajengea uwezo TRA katika ukusanyaji kodi

KOKU DAVID-DAR ES SALAAM

Chuo cha Kodi nchini (ITA), kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Misaada la Japan (JICA), mwishoni mwa wiki iliyopita wameendesha mafunzo ya utozaji wa kodi katika sekta ya ujezi kwa watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Naibu Mkuu wa Chuo cha ITA, Dk Lewis Ishemoi amesema mafunzo hayo ni muendelezo wa mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa TRA katika ukusanyaji wa kodi katika sekta maalum za Ujenzi, mawasiliano, madini, mafuta na gesi ambazo zinakua kwa kasi.

Amesema mafunzo hayo yataisaidia TRA kuwa na wataalamu waliobobea katika ukusanyaji wa kodi pamoja na kuongeza makusanyo hasa katika sekta ya ujenzi ikiwa ni pamoja na kuuelewa mfumo mzima wa ujenzi, kufahamu mnyororo wa thamani pamoja na wadau wakuu katika shughuli za ujenzi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles