25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Irene Uwoya: Nitayaanika maisha yangu hivi karibuni

iRENE uWOYANa Rhobi Chacha
MWIGIZAJI Irene Uwoya amesema anajiandaa kuweka wazi historia yake ya maisha maana kuna watu wanapotosha mashabiki wake kwa taarifa za uongo ambazo hazina uhusiano na maisha yake halisi.
Uwoya amesema atafanya hivyo kwa kuwa anataka mashabiki wake waelewe maisha yake halisi na wawapuuze wanaompakazia kwa historia za ajabu zenye lengo la kumchafua na kumrudisha nyuma katika kazi zake na uhusiano wake wa kimapenzi.
“Nitayaanika maisha yangu halisi ili wote wanielewe vema na waachane na kunichukulia tofauti, maana naamini najijua mwenyewe nilikotokea na namna ninavyoishi, hivyo nitaweka wazi ili watu watambue maisha yangu na sipendi watu wanizungumzie kwa kuwa hawayajui maisha yangu,’’ alieleza Uwoya.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles