33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Irene Uwoya aula viti maalum

f7d8b2e2ec0fec94d7385f158c725b9dNA BAKARI KIMWANGA, DODOMA

MSANII pekee wa Bongo Movie, Irene Uwoya, ameibuka kidedea kwenye uteuzi wa wagombea ubunge wa viti maalumu uliokamilishwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) jana.

Uwoya alipata nafasi hiyo baada ya jina la mtoto wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, ambaye pia ni mgombea wa CCM katika jimbo la Ubungo, Dk Didas Masaburi, Juliana Masaburi kukatwa.

Mtoto huyo wa Masaburi, alishinda kura za maoni kupitia kundi la Vijana akiwakilisha Mkoa wa Mara lakini baada ya kukatwa nafasi yake ikachukuliwa na Irene Uwoya.

Awali mwigizaji huyo aliibuka kidedea kwenye kura za maoni jimbo la Tabora mjini kwa kupata jumla ya kura 34 akafuatiwa na Mariam Khamis aliyepata kura tatu na Zahara Michuzi aliyeambulia kura mbili.

Uwoya anakuwa msanii pekee wa Bongo Movie aliyeshinda nafasi hiyo baada ya wasanii wenzake, Wema Sepetu, Keysher na Steven Mengele (Steve Nyerere) kuangushwa kwenye ngazi tofauti.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles