30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Infantino ataka timu 48 Kombe la Dunia

Gianni Infantino
RAIS wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA),Gianni Infantino

ZURICH, USWISI

RAIS wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA),Gianni Infantino, amependekeza kuongezwa kwa timu za mataifa 16 kutoka 32 zinazoshiriki  michuano ya Kombe la Dunia.

Idadi hiyo itafanya kuwapo kwa timu 48 ambazo  ni zaidi ya ahadi yake ya awali alioitoa katika kampeni za urais wa Fifa ambapo alitaka michuano hiyo kushirikisha jumla ya timu 40.

Kwa mujibu wa  Infantino  (46), anaeleza kuwa  mataifa 16 yataondolewa katika mzunguko wa kwanza na kubakia mataifa 32 yatakayoshiriki hatua ya makundi ikifuatiwa na hatua zaidi ya mtoano.

Infantino alisema uamuzi wa kupanua michuano hiyo mikubwa duniani  inatarajia kufanyika Januari mwakani.

“Tupo mbioni kutafuta  njia sahihi ya kuboresha michuano hii na kabla ya kufika katika uamuzi, kwanza tutafanya mdahalo mwezi huu wa kujadili  hoja hii.

Infantino alisema  kwa sasa timu 32  kutoka katika mataifa mbalimbali zitashiriki katika hatua za  awali za mtoano  na washindi kujiunga na timu 16 washindi  wa  hatua ya makundi.

“Kwa sasa tunaendelea na utaratibu wa kawaida wa Kombe la Dunia kwa kuwa na timu za mataifa 32, lakini hapo baadaye tunatarajia kuwa na timu 48.

“Wazo la Fifa ni kuendeleza soka katika mataifa yote, dunia ni kubwa hivyo tunataka kufanya mashindano haya yawe zaidi na yalivyokuwa hapo awali,” alisema Infantino ambaye alichukua nafasi ya Rais wa Fifa wa zamani, Sepp Blatter, Januari 26, mwaka huu.

Infantino aliongeza kuwa  wazo hilo litapanua mashindano hayo kwa kuwa yatashirikisha mataifa ambayo hayakupata nafasi hapo awali.

Katika wazo hilo jipya, inadaiwa  huenda  ikatokea England kucheza dhidi ya Iceland katika mzunguko wa kwanza kama England hawakufuzu moja kwa moja.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles