27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Hussein Machozi: Sijafaidika na muziki

Jessca Nangawe

MKONGWE wa muziki wa kizazi kipya Hussein Machozi amesema licha ya kuanza muda mrefu muziki lakini hajawahi kunufaika zaidi ya kumwezesha kununua simu ya shilingi elfu 60.

Akizungumza Hussein alisema kwa miaka yote tangu aanze kuimba amekua akifanya kazi hiyo kama sehemu ya kujiburudisha na si kumwingizia kipato kama ilivyo kwa wengine.

“Muziki upo kwenye damu yangu, ukweli sijawahi kunufaika nao, nakumbuka pesa niliyotumia kutokana na muziki wangu ni elfu 60 ambayo nilinunulia simu na siwezi kujutia kwa lolote,” alisema Hussein.

Msanii huyo aliongeza kwa kusema, ameonekana kuwa kimya lakini ukweli ni kwamba amekua akibanwa na majukumu mengine ya maisha lakini sio kweli kwamba ameacha muziki.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles