31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Hemedi: Sifikirii kurekodi video nje ya nchi

hemedi_suleiman_06NA THERESIA GASPER

MSANII wa muziki wa kizazi kipya na filamu za kibongo nchini, Hemedi Suleiman ‘PHD’, amesema hajawahi kufikiria kufanya video za nyimbo zake nje ya nchi kama wafanyavyo baadhi ya wasanii wenye kipato cha juu.

Hemedi, ambaye kwa sasa anatamba na kibao chake cha ‘Memories’, alisema anachofikiria ni kushirikiana na wasanii kutoka nje na si kufanya video nje ya nchi wakati nchini kuna mazingira ya kutosha kunogesha video zake.

“Kitu ambacho kipo kichwani mwangu kwa sasa ni kufikiria kufanya kazi na wasanii wa nje, ili niweze kuupaisha muziki wangu kimataifa zaidi na kuweza kuitangaza vyema Tanzania, sifikirii video za nje,” alisema.

Hemed anatarajia kuachia video yake mpya ya ‘Memories’ alioufanyia katika mazingira ya nchini chini ya usimamizi wa studio ya Downvilla records.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles