27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Hatima ya Kibonde mikononi mwa Polisi

Mtangazji maarufu wa redio nchini, Ephraim Kibonde
Mtangazji maarufu wa redio nchini, Ephraim Kibonde

Na Asifiwe George, Dar es Salaam

KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillus Wambura, amesema Jeshi hilo kwa sasa lipo katika uchunguzi dhidi ya mtangazaji wa Kituo cha Redio cha Clouds FM, Ephraim Kibonde na mwenzake, Gadna Habash wa Times FM, ambao wameachiwa huru kwa dhamana.

Kamanda Wambura aliliambia MTANZANIA jana kwamba baada ya uchunguzi huo, iwapo watapatikana na hatia, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao, ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.

Kwa mujibu wa Kamanda Wambura, Kibonde na Gadna wanadaiwa kutenda makosa matano, ikiwamo kusababisha ajali, kukimbia, kutotii amri halali ya Polisi, kukimbia na trafiki ndani ya gari, kutoa lugha chafu kituoni pamoja na kukataa kupima ulevi.

Alisema watangazaji hao waliyatenda makosa hayo siku ya Jumamosi saa 12 asubuhi, katika eneo la Makumbusho, ambapo Kibonde akiwa anaendesha gari walilokuwa wamepanda aliligonga gari la raia mmoja wa kigeni (Mzungu) na kukimbia.

Jana MTANZANIA lilishuhudia askari wa usalama barabarani wakiwa wameongozana na Kibonde pamoja na raia huyo wa kigeni katika eneo la tukio ambapo walikuwa wakipima ajali hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles