23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA CHINI YA CHADEMA YATOA MIKOPO YA 624M/- KWA WANAWAKE NA VIJANA

mikopo-arusha

Halimashauri ya jiji la Arusha imetoa jumla ya Tshs milioni 624, ambazo kati ya hizo milioni 425 ni kwa ajili ya wanawake na milioni 199 kwa ajili ya vijana na hii ni awamu ya pili kwa Halmashauri kutoa mikopo kwa ajili ya vikundi mbalimbali.

Mara ya kwanza jumla ya milioni 405 zilitolewa, hivyo mpaka sasa jumla ya bilioni 1.24 zimetolewa kama mikopo kwa vikundi vya vijana na wanawake.

Mikopo hiyo ambayo ni mapato ya ndani ya Halmashauri ambayo ni zaidi ya 1bil kila mwezi,sambamba na hilo Halmashauri imetoa mafunzo maalum kwa ajili ya matumizi bora ya fedha hizo.

Kwa mujibu wa Halmashauri, bado itaendelea kutoa mikopo hiyo kwa wananchi wote wa Jiji la Arusha ambao kwa sasa wameshauriwa kuunda vikundi ili waweze kufaidika na mikopo hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles