24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

GWAJIMA: NITASHIRIKIANA NA POLISI

ASKOFU wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, amesema ameitikia wito uliotolewa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam ya kumtaka kuripoti katika kituo hicho saa tatu asubuhi.

Akizungumza na waandishi wa habari Kituo Kikuu cha Polisi jana, alisema kwa sababu ni wito halali uliotolewa na polisi, hivyo basi ataendelea kushirikiana na jeshi hilo ili kuhakikisha kuwa suala hilo linakwisha.

“Nilikuwa miongoni mwa washukiwa wa dawa za kulevya, lakini walinipima na ‘kusachi’ nyumbani kwangu hawajakuta chochote, hivyo basi nitaendelea kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha kuwa washukiwa wa dawa hizo  wanafikishwa kwenye mikono ya sheria,” alisema Gwajima.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles