24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Gavana afichua siri upotevu fedha mitaani

Profesa Benno Ndullu
Profesa Benno Ndullu

NA JONAS MUSHI, DAR ES SALAAM

GAVANA wa Benki Kuu (BoT), Profesa Benno Ndullu, amekiri kupotea kwa fedha kwenye mikono ya watu na kueleza hali hiyo imesababishwa na fedha kuhama kutoka katika mikono haramu.

Asema hali hiyo imechagizwa na uamuzi wa Serikali kubana shughuli za watu ‘misheni town’ na badala yake fedha zimekwenda kwenye matumizi halali na sahihi kwa umma.

Kauli hiyo aliitoa jana jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, ambapo alisema pamoja na hali hiyo hakuna mdodoro wa uchumi.

Profesa Ndullu alifananisha kipindi cha sasa na kile kilichoitwa ‘ukata’ enzi za utawala wa Rais wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa, wakati anapambana na rushwa na kusema kwamba alifanikiwa kuinua uchumi.

Alisema Serikali imechukua hatua kubwa ya kuongeza mapato kwa kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kuziba mianya ya ukwepaji wa kodi.

“Serikali katika matumizi yake imebana shughuli za wale waliokuwa wa ‘misheni town’ na sasa shughuli hizi zinafanyika kwa uwazi na kwa uhalali.

“Kiuchumi hakuna fedha iliyopotea bali fedha zimehama na kwenda kwa wale wanaofanya shughuli za kuhudumia umma kiuhalali na tunaita ‘redistribution’ (mabadiliko ya mgawanyo).

“Ila wapo watakaolalamika kwamba fedha zimepotea. Wale ambao walikuwa wanapata fedha kwa shughuli ambazo Serikali imezibana hatuwezi kusema fedha haijapotea. Ni kweli kwa wao fedha imepotea, lakini kitaifa fedha haijapotea.

“Katika kutambua fedha haijapotea tunaangalia fedha zinazotolewa na BoT, ambapo katika kila Sh 100 inayotolewa Sh 36 huwa zinaenda mikononi mwa mabenki na taasisi za fedha, wakati Sh 64 zinakuwa mikononi mwa watu na nje ya mfumo, hakuna mabadiliko makubwa katika hilo,” alisema.

Profesa Ndullu alisema kinachoelezwa kwamba ni kupungua kwa fedha zinazopelekwa benki, kumetokana  na  Serikali  kuhami sha uwekaji wa fedha za mashirika yake kutoka katika benki binafsi na kwenda BoT.

Alisema sababu za  kufanya hivyo ni kuweka wazi mapato na matumizi ya mashirika ya Serikali.

Hata hivyo alisema si kwamba fedha hizo hazirudi kwenye benki za biashara kwani hufanya malipo kwa mashirika kupitia benki hizo.

“Wakati wa matumizi huwa tunatumia benki hizo si kwamba tunalipa moja kwa moja kwenye mashirika yetu,” alisema.

KUPOROMOKA UCHUMI

Akizungumzia kuhusu dhana ya kuporomoka kwa uchumi alisema kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka huu uchumi umekua kwa asilimia 5.5.

“Kiuchumi ukuaji huo tunaufananisha na wa mwaka jana kipindi kama hicho ambapo kwa mwaka jana ulikua kwa asilimia 5.7 hivyo kuna mabadiliko kidogo,” alisema Prof. Ndulu.

Alisema wapo watu waliotafsiri tofauti hiyo kuwa itaathiri ukuaji wa uchumi kwa mwaka suala am- balo si sahihi.

“Robo ya kwanza ya mwaka jana ukuaji ulikua asilimia 5.6 lakini ukuaji wa mwaka ukawa asilimia 6.9. Tunatarajia ukuaji wa mwaka huu utakuwa asilimia 7.2 kutokana na viashiria ambavyo tunaviona,” alisema.

VIASHIRIA

Alitaja viashiria hivyo kuwa ni ukuaji wa uzalishaji wa umeme kwa asilimia 14.5 katika kipindi cha nusu mwaka (Januari-Juni 2016) ambapo uzalishaji umefikia kWh trilioni 3.4 kutoka kWh trilioni 3.0.

Kiashiria kingine ni kuongezeka kwa uzalishaji na matumizi ya saruji kwa asilimia 7 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka huu. “Pia  kuna  ongezeko  la  mali ghafi za viwandani kutoka nje kwa asilimia 19 na hii inaonyesha kuwa ukuaji wa viwanda unaenda kwa kasi.

Aliongeza  viashiria  vingine ni kuongezeka kwa mauzo ya nje ya bidhaa za viwandani kwa asilimia 15.6, kuongezeka kwa makusanyo ya kodi na kuongezeka kwa mikopo inayotolewa na mabenki ya biashara kwa Sh trilioni 1.1 kip- indi cha nusu mwaka.

MIRADI MIKUBWA

Profesa  Ndullu  alisema  uwepo wa miradi mikubwa inayotarajiwa kuanza mwaka huu ni kiashiria mojawapo  cha  ukuaji  mzuri  wa uchumi.

Alitaja baadhi ya miradi kuwa ni ujenzi wa reli ya kati km 200, ujenzi wa bomba la mafuta ku- toka Uganda hadi Tanga, ujenzi wa bandari ya Dar es Salaam, ujenzi wa kituo cha biashara Kurasini, ujenzi wa mitambo ya kufua umeme ya Kinyelezi II, upanuzi wa viwanja vya ndege na ujenzi wa maghala ya kuhifadhia chakula.

Alisema miradi hiyo itatumia fedha nyingi, mali ghafi zinazozalishwa pamoja na kutumia nguvu kazi hivyo kutoa ajira nyingi.

DENI LA TAIFA

Profesa Ndullu alisema deni la Taifa, mfumuko wa bei na thamani ya shilingi ni miongoni mwa mambo yanayoonyesha hali ya uchumi ilivyo na Serikali inafanya vizuri katika mambo hayo.

Akizungumzia kuhusu deni la taifa alisema licha ya kuendelea kuongezeka bado ni stahimilivu likilinganishwa na pato la taifa.

“Kwa kuangalia uwiano wa mapato na deni la taifa  bado ni stahimilivu na kwa asilimia 20 ya pato la taifa na ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 50,” alisema Profesa Ndullu na kusisitiza: “Bado tuna nafasi kubwa ya a kukopa bila kuathiri ustahilivu wetu.”

Alisema licha ya deni hilo kuendelea kuongezeka lakini kasi ya kuongezeka imepungua kwa kipindi cha nusu mwaka hususani deni la nje ambalo limeongezeka kwa asimilia 2.6 tu kufikia Juni mwak huu kutoka Desemba mwaka jana.

Hata hivyo alisema deni la ndani limezidi kuongezeka kwa kasi zaidi na kufikia zaidi ya Sh bil- ioni 10 hadi Juni mwaka huu kuto- ka bilioni 8 Desemba mwaka jana.

Kuhusu mfumuko wa bei alisema uko vizuri kwani kwani Agosti mwaka huu umefikia asilimia 4.9 ikilinganishwa na asilimia 6.8 Desemba mwaka jana.

Kwa upande wa mwenendo wa thamani ya shilingi ya Tanzania alisema imeendelea kuwa tulivu katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016.

“Mpaka sasa mfuko wa bei ni asilimia 4.9 ambao uko vizuri na tunaendelea kuudhibiti. Tanzania ni kati ya nchi 10 za Afrika ambazo uchumi wake unakuwa vizuri. Lakini pamoja na hali juhudi zimefanyika kudhibiti matumizi hivyo kufanya bajeti kutekelezwa bila tatizo,” alisema Profesa Ndulu

Gavana Ndullu alisema akiba ya fedha za kigeni ni Dola za Marekani bilioni 4, ambazo zinaweza kuhudumia mahitaji ya bidhaa na huduma
kutoka nje kwa miezi minne.  Septemba 6, mwaka huu Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alitoa maazimio ya kikao cha Kamati Kuu ambapo chama hicho kilijadili hali ya uchumi nchini.

Alisema kwa kipindi ambacho Rais Magufuli amekuwa madarakani kasi ya ukuaji wa uchumi ambayo ilikuwepo awali imepungua kwa asilimia nne kutoka asilimia tisa hadi asilimia tano, jambo ambalo halijawahi kutokea kwa kipindi kirefu katika historia ya Tanzania.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles