27.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Future kulipa Mil 7 kwa mwezi

NEW YORK, MAREKANI 

RAPA Nayvadius Wilburn maarufu kwa jina la Future, ametakiwa kila mwezi kuweka mezani kiasi cha dola 3,200, ambazo ni zaidi ya milioni 7 za Kitanzania kwa ajili ya huduma kwa mtoto wake Reign. 

Mama wa mtoto huyo Eliza Reign Seraphin ameshinda kesi hiyo ambayo ilianza kunguruma mapema mwaka huu ambapo awali mrembo huyo alikuwa anataka apewe dola 53,000, zaidi ya milioni 122 kwa mwezi. 

“Tuna imani kwamba, kama tutafanikiwa kupata nyaraka zake kama vile zile za benki, kadi, kiasi cha fedha kwa ajili ya huduma ya mtoto itaongezeka,” alisema mwanasheria wa mama wa mtoto. 

Mrembo huyo na mwanasheria wake wamekataa kuwa, rapa huyo amekuwa akiingiza kiasi cha dola 30,000 kwa mwezi zaidi ya milioni 69, hivyo hawezi kutoa kiasi kikubwa cha fedha. 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles