30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

EU: Mkataba wa Brexit unaweza kufikiwa wiki hii

Brussels, Ubelgiji

UMOJA wa Ulaya (EU) umesema mkataba wa Brexit unaweza kufikiwa wiki hii, lakini mapendekezo ya Serikali ya Uingereza hayajitoshelezi kuwezesha kupatikana kwa makubaliano.

Mwakilishi Mkuu wa Umoja wa Ulaya kwenye mazungumzo ya Brexit, Michael Barnier, alisema kuelekea mkutano wa mawaziri wa mambo ya kigeni wa umoja huo, changamoto kubwa ni kubadili mapendekezo ya Uingereza kuhusu suala tata la mpaka wa Ireland mbili kuwa mkataba.

Kuhusu matarajio ya mkutano huo, Barnier alisema hata kama mkataba utakuwa mgumu, unawezekana kufikiwa wiki hii.

Viongozi wa Umoja wa Ulaya watakutana kwa mkutano wa kilele wa siku mbili mjini Brussels kuanzia Alhamisi huku suala la Brexit likitarajiwa kuwa mada kuu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles