31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

DJ Spinall aja na Remix ya ‘Sere’ aliyomshirikisha Fireboy

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Baada ya kutoa albamu yake ya tano ‘GRACE’ (kupitia TheCapMusic) na nyimbo nyingi, msanii aliyeshinda tuzo kibao, mtayarishaji na mtunzi wa nyimbo, DJ Spinall amerudi na remix ya wimbo wake wa ‘Sere’ akiwa na Fireboy DML na 6lack ambaye ni mshindi wa Tuzo ya Grammy – Mwimbaji wa alt-R & B wa Amerika.

Black anaongeza joto la ziada kwenye wimbo huo ambao tayari umeonekana kuwa kuwavutia mashabiki kutokana na mchanganyiko wa kupendeza wa sauti za nguvu za Afropop na Hi-Life, Hip-Hop na R&B.

GRACE albamu ambayo ni mradi wa nyimbo 15 ambayo ndani yake kuna kolabo za nguvu na wasanii Kranium kwenye ‘Dis Love’, Tiwa Savage na Wizkid; Omah Lay, Niniola, WurlD, Shaybo, Benjiflow, Oxlade na wengine wengi. DJ Spinall alipata umaarufu kwa mara ya kwanza mwaka 2004 kama mtangazaji wa redio, kabla ya kuzindua studio na kampuni ya usimamizi ya TheCAPMusic mwaka 2014.

Mwaka 2017 alikuwa DJ rasmi wa Tuzo za BET na baadaye mwaka 2019 alikuwa DJ wa kwanza wa Nigeria kutumbuiza kwenye Tamasha la Glastonbury.

Aidha, baadaye mwaka 2019 alifanya onyesho jingine lililoitwa XOYO, jijini London, Uingereza. Amezuru miji kadhaa ya Amerika ikiwa ni pamoja na New York, Miami, Austin na Washington DC

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles