25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Diamond Platnumz atoa neno kwa wasanii

BRIGHITER MASAKI, DAR ES SALAAM

STAA wa muziki nchini, Naseeb Abdul, ‘Diamond Platnumz’ amewataka wasanii wenzake kutumia vivutio vya Taifa katika kazi zao ili kutangaza utalii uliopo nchini.

Diamond Platnumz amesema kwa upande wake yupo tayari kutangaza vivutio mbalimbali kwa ajili ya kuitangaza nchi yake kupitia kazi zake.

“Haiwezekani mastaa kutoka nchi zingine kutembelea vivutio vyetu wakati sisi wenyewe tupo karibu na tunashindwa kwenda, mastaa wengi wamekuja nchini kama vile David, Beckham, Lionel Messi wamepanda mlima wetu Kilimanjaro.

“Nimefurahi kupanda Kilimanjaro japokuwa sikufanikiwa kufika kileleni, lakini kwangu ni jambo la kubwa na historia, hivyo wasanii kupitia kazi zetu inabidi tutangaze vivutio vyetu ili watalii waje, nchi ijulikane na tukuze uchumi wetu,” alisema msanii huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles