31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Demi Lovato kuitambulisha ‘Big Ballad Style’

New York, Marekani

NYOTA wa muziki nchini Marekani, Demi Lovato, ameweka wazi kuwa, anatarajia kuimba wimbo wake, Big Ballad Style ambao aliuandika na kuurekodi siku nne kabla ya kupoteza fahamu kutokana na utumiaji wa dawa za kulevya.

Mwaka 2018, mrembo huyo mwenye miaka 27, alikimbizwa hospitalini baada ya kukutwa ndani kwake akiwa amepoteza fahamu baada ya kutumia dawa za kulevya.

Baada ya kupewa matibabu, msanii huyo alipelekwa kituko cha matibabu ya dawa hizo na kukaa huko kwa siku 90.

 “Nianze kwa kumshukuru Mungu kuniweka hai hadi kufikia hapa, lazima niwe muwazi kwenye safari yangu hii ngumu ya dawa za kulevya, hivyo kwenye tuzo hizi za Grammy natarajia kuimba wimbo huo,” alisema msanii huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles