27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

DAWA ZA KUPUNGUZA MAKALI YA VVU ZABORESHWA ZAIDI ULAYA, AMERIKA

gallery

Watafiti nchini Uingereza wanasema dawa za kupunguza makali ya virusi katika Ulaya na Amerika ya Kaskazini zimeboreshwa kiasi kwamba watu mwenye Virusi vya UKIMWI wanaweza kuishi kwa karibia sawa tu na watu wengine wasio na virusi.

Wanasayansi kutoka Chuo kikuu cha Bristol, waliwachunguza watu wenye virusi vinavyosababisha UKIMWI wapatao elfu tisini. Makadirio yao yanaonesha kuwa mtu mwenye umri wa miaka 21 aliyeanza matibabu mwaka 2008 au baadaye anaweza kuishi mpaka kufikia umri wake wa miaka 70.

Zaidi ya watu milioni mbili wanaishi na Virusi vya UKIMWI katika Ulaya na Amerika Kaskazini.

Kwa upande wa Takwimu za ulimwengu, watu walioathirika na virusi hivyo ni milioni 36 wengi wao wakiwa barani Afrika.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles