23 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Davido kuja na albamu mpya Julai

LAGOS, NIGERIA 

STAA wa muziki nchini Nigeria, David Adeleke, maarufu kwa jina la Davido, amewataka mashabiki zake kujiandaa na ujio wa albamu yake mpya Julai mwaka huu.

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 27, ameliweka wazi jina la albamu hiyo kuwa ni ‘A Better Time’ hivyo mashabiki wakae tayari kusapoti kazi hiyo.

“Julai mwaka huu nitaachia albamu mpya ambayo inajulikana kwa jina la “A Better Time.” Mashabiki kaeni tayari kusapoti kazi hiyo,” aliandika msanii huyo.

Hata hivyo, alikwenda mbali zaidi kwa kuwadokeza mashabiki hao kuwa, ndani ya albamu hiyo kuna wimbo ambao amefanya na rapa wa kutoka nchini Marekani, Nicki Minaj.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles