23.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Daktari: binadamu huzaliwa na mifupa 300

AVELINE KITOMARY – DAR ES SALAAM

Daktari Bingwa wa Upasuaji Mifupa na Magonjwa ya Ajali  kutoka Taasisi ya Tiba na Mifupa Muhimbili (MOI), Dk. Kennedy Nchimbi amesema binadamu huzaliwa akiwa na mifupa 300 lakini anapokuwa mtu mzima huungana na kuwa 206

Dk. Nchimbi amesema baadhi ya mifupa hiyo kuungana na kutengeneza  mifupa mikubwa.

Dk. Nchimbi amesema ukomavu wa mifupa (Ossifications), kwa kawaida binadamu anapokuwa mtu mzima wa miaka 25 mifupa hiyo huungana kwani anapokuwa mdogo mifupa ina kuwa imeachana hivyo anavyozidi kukua ndivyo inavyoungana.

Amesema kuna sehemu mifupa inakuwa haijafunga hivyo ikihesabiwa inakuwa mingi zaidi na baadae zinaungana kwa kuwa ni za ukuaji ndio maana hurefuka.

“Zaidi ya nusu ya mifupa ya mwili wa binadamu ipo kwenye mikono na miguu na kati ya mifupa 206 mifupa 106 ipo kwenye mikono na miguu,” amesema Dk. Nchimbi.

Aidha ameeleza kwamba sehemu ambazo zinagawanyika kabla ya kukomaa zinaruhusu  kukua (Growth plates  epiphyceal plate), mfano  mfupa wa paja kabla ya miaka 25 binadamu wa kawaida  mfupa huo unaweza kuwa na sehemu tatu hadi nne  tofauti lakini ukubwani huonekana mmoja tu.

“Ndio maana  hata mtoto anapozaliwa  fuvu la kichwa  unaweza kulibana  na huwezi kufanya hivyo  baada ya kukomaa   hata akina mama wanaopitiliza siku za kujifungua yaani wiki 40, hawezi kujifungua kwa njia ya kawaida  ina kuwa ni shida,”namesema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles