25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Chuo cha St. John chaanza kutumia mfumo wa kidigital kufundisha

Na Ramadhan Hassan, Dodoma

Chuo Kikuu cha St. John cha jijini hapa kimesema kimeanza kutumia mfumo wa kufundisha kidigital (E-learning) ambapo kimedai  umekuwa  na mafanikio makubwa.

Hayo yalielezwa jana na Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Yohana Msanjila alipokuwa akizungumza katika mahafali ya 11 ya chuo hicho .

Katika mahafali hayo, chuo hicho  kimewatunuku Shahada mbalimbali jumla ya wahitimu 1322 ambapo kati yao wahitimu 631 ni wa kike sawa na asilimia 47.7 ya wahitimui wote na wanaume ni 691 sawa na asilimia 52.3.

Prof. Msanjila alisema katika mahafali ya mwaka jana chuo kilieleza azma yake kukibadilisha na kutumia mfumo wa kidigitali ambapo alidai mpango huo ulilenga kuwekeza zaidi katika mifumo ya Tehama ili kuweza kutoa mafunzo kwa wanafunzi kwa njia ya kisasa zaidi.

“Napenda kuifahamisha hadhara hii kuwa mpango wetu unakwenda vizuri katibu wahadhiri wote wamepatiwa mafunzo  kwa nyakati tofauti mafunzo hayo yamewezesha kozi nane.

“Kupitia ‘moodle’  wahadhiri na wanafunzi  sasa wanakutana mtandaoni  na kufanya mambo yote yanayotakiwa  kufanyika katika ufundishaji na ujifunzaji  wa darasa la kawaida hii  ni kuesema kuwa mwalimu anaweza kufundisha,kutoa majaribio,kutoa mitihani kusahihisha na kutoa matokeo humo humo mtandaoni,”alisema Prof. Msnjila.

Alisema mpango wa kufundisha kidigital   unaenda sambamba na mpango wa kuimarisha utumiaji wa E-Library kwa ajili ya kuwezesha wanafunzi na wafanyakazi  waweze kusoma vitabu  na nyaraka mbalimbali  muhimu hupitia online.

“Ili kufanikisha mpango huo chuo kimeongeza uwezo wa bandwidth kutoka mb 20  hadi kufikia 40 ili kuwezesha wanafunzi na walimu kusoma kwa wepesi,”alisema.

Alisema chuo kinaendelea na mchakato wa kumalizia kuandaa program mpya ya BSc in IT ambayo itakuwa ni kichocheo cha kutumia mbinu za kidijitali.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho, Prof. Penina Mlama alisema katika mwaka huu wa fedha chuo kimepanga jingo la utawala ambapo alidai ujenzi huo unalenga kuongeza idadi ya ofisi kwa wafanyakazi wake kutokana na ongezeko la wanataaluma.

“Hivi sasa tuna uhaba wa Ofisi kwa wafanyakazi wetu jambo linalofanya wafanyakazi kushirikiana kukaa ofisi moja,kukamilika kwa jengo hilo kutapunguza tatizo la uhaba wa ofisi kwa wafanyakazi wetu,”alisema Prof. Penina.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo hicho, Askofu Mkuu mstaafu, Donald Mtetemela alisema chuo kinafanya kila kiwezavyo kuendeleza mahusiano ya kitaaluma na vyuo mbaloimbali ndani ya nchi na nje ya nchi.

Alivitaja vyuo hivyo kuwa ni pamoja na Kenyatta University, University of London, Norwegian na Danish Institute for international studies.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles