23 C
Dar es Salaam
Monday, August 15, 2022

CHANJO YA NYOKA YAISHTUA SERIKALI

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu

NA Mwandishi Wetu-DAR ES SALAAM

SERIKALI imewaagiza waganga wakuu wa mikoa na viongozi wa hospitali zoteĀ  kuhakikisha wanaingiza chanjo ya nyoka katika mfumo wa dawa za dharura.

Taarifa ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini- Afya, Nsachris Mwamwaja, ilisema agizo hilo linatakiwa kutekelezwa mara moja.

Taarifa hiyo, imewaagiza waganga wakuu wa mikoa na halmashauri zote kupitia kwa uangalifu takwimu za wagonjwa waliong’atwa na nyoka kuanzia mwaka 2013 hadi 2016.

Aliwataka kuwasilisha takwimu hizo wizarani kabla ya Januari 31, mwakani.

ā€œKama tunavyofahamu, nchi yetu ina aina mbalimbali za nyoka ambao pindi wakimuuma mtu huleta madhara ya kiafya, tunafahamu Ā tatizo hili lipo zaidi maeneo ya vijijini ambako uwezo wa wananchi kumudu gharama za matibabu ni mdogo.

ā€œDawa za kutibu sumu ya nyoka huagizwa kutoka nje ya nchi. Dawa hizo siyo tu hazipatikani kwa urahisi, bali pia zinapatikana kwa gharama kubwa,ā€ ilieleza taarifa hiyo.

Pia taarifa hiyo, ilisema bei ya kununulia dawa hizi ni kati ya Dola za Marekani 55 hadi 85 sawa na Sh 118,250 hadi 182,750 kwa chupa dogo (vial).

ā€œKichupa hiki hutumika kwa wagonjwa wanne, baada ya kufunguliwa dawa hiyo huwa haifai tena kutumika ndani ya mwezi mmoja tu,ā€ ilisema taarifa hiyo.

Pamoja na changamoto hizo, Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) kila mwaka huagiza dawa hizo kwa ajili ya mahitaji ya kutibu wagonjwa walioumwa na nyoka, ambapo bei ya kuinunua kutoka MSD ni ShĀ  200,000 kwa chupa kimoja.

ā€œHospitali zetu mbalimbali zimekuwa zikiagiza dawa hizi kutoka MSD na kwa washirika Ā wengine kwa bei hii au zaidi na kuwatibu waathirika wanaohitaji dawa za sumu za nyoka mara zinapohitajika,ā€ iliongeza taarifa hiyo.

Aliongeza ā€œKwa mujibu wa Sera ya Afya ya mwaka 2007, huduma za tiba hutolewa bure kwa makundi maalumu au kwa kuchangiwa kwa sehemu ya gharama, au kwa kupitia mfumo wa bima mbalimbali za afya.

ā€œKwa wale wasio na uwezo na wanaothibitishwa kuwa hawana uwezo, utaratibu wa msamaha hutumika. Hivyo tukipata takwimu sahihi zitatusaidia kujua mahitaji halisi ya dawa ya sumu ya nyoka nchini. Itasaidia kuboresha upangaji, uagizaji na upatikanaji wa dawa hizo nchini,ā€ alisema.

Pia MSD Ā imetakiwa kuweka utaratibu wa haraka wa kununua dawa hizo moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji ili kupata unafuu wa bei,ā€ alisema.

Kutokana na hali hiyom Ā Watanzania wamehimizwa Ā kukata bima ya afya kwa sababu zinapunguza gharama.

ā€œWajiunge na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) au Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ili kupata unafuu wa matibabu haya na mengine.

ā€œMfano gharama ya kujiunga na CHF katika halmashauri mbalimbali kwa kaya ni kati ya Sh 5,000 Ā hadiĀ  30,000 kwa mwaka…

ā€œKwa wagonjwa ambao watakuwa na bima ya afya, gharama za matibabu hayo zitalipwa kwa kupitia utaratibu huo wa Bima,ā€ alisema.

Wagonjwa ambao hawatakuwa na bima ya afya, watatakiwa kuchangia gharama hiyo kwa nusu ya bei ya gharama ya dawa hizi au kwa kiwango kingine kitakachoamuliwa na Mganga Mkuu wa Serikali kadri itavyohitajika.

ā€œHii ni kutokana na ukweli kwamba kung’atwa na nyoka ni ajali na wananchi wengi wanaopatwa na ajali hii wapo maeneo ya vijijini ambao kimsingi uwezo wao wa kumudu gharama hizi kubwa za matibabu ya dawa ya sumu ya nyoka ni mdogo,ā€ilisema taarifa hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
198,784FollowersFollow
550,000SubscribersSubscribe

Latest Articles