24.3 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

CHAINZ AMNUNULIA MAMA YAKE NYUMBA NYINGINE

NEW YORK, MAREKANI


MSHINDI wa tuzo za Grammy nchini Marekani, Tauheed Epps ‘2 Chainz’, amemnunulia mama yake nyumba ya pili baada ya mafanikio yake ya muziki kuwa makubwa.

Msanii huyo kutoka Atlanta, alimnunulia mama yake nyumba ya kwanza mwaka 2012.

“Mwaka 2012 nilimnunulia mama yangu nyumba kutokana na kiasi cha fedha nilichokuwa nikikipata wakati huo, sikuwa na uhakika kama mafanikio yangu yangekuwa makubwa mwaka huu, lakini sasa kipato changu kimezidi kukua.

“Sina ambacho naweza kumfanyia mama yangu nikafikia yale aliyonitendea, hivyo atakuwa anafurahia mafanikio yangu, nimeona bora nimnunulie nyumba nyingine kwa kuwa nampenda sana,” aliandika 2 Chainz kwenye ukurasa wake wa Instagram.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles