23.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

CEO NMB Ruth Zaipuna ‘ashine’ tuzo ya Mkurugenzi Mtendaji Bora wa Kibenki Afrika 2022

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, mwishoni mwa wiki alitangazwa kuwa mshindi wa kipengele cha Afisa Mtendaji mkuu Bora Africa kwa Mwaka 2022 (Tanzania) katika kipengele cha benki na Uongozi wakati wa hafla iliyofanyika Ijumaa, Mei 27, 2022 katika hoteli Movenpick jijini Nairobi, Kenya.

Tuzo hiyo ilitolewa na Julias Alego Mkurugenzi Mtendaji Tasisi ya Mabenki nchini Kenya na kupokelewa na Mweka Hazina Mkuu wa benki ya NMB, Aziz Chacha.

Akipokea tuzo hiyo kwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, Chacha alisema, “Ni heshima kubwa sana kuwa nanyi usiku wa leo kupokea Tuzo ya ‘African Banking CEO of the Year 2022 (Tanzania)” kwa niaba ya Zaipuna, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Plc,”

Mara baada ya kupokea Tuzo Hiyo kwa niaba ya CEO wa NMB, Aziz Chacha alitoa tuzo hiyo kwa wafanyakazi wa NMB kwa kujitolea kwao na nia ya kuendelea kuwa mstari wa mbele wa vumbuzi, kuzingatia wateja, uthabiti, uaminifu, na usalama. 

“Kwa maneno ya Ruth, natoa tuzo hii maalum kwa moja ya mtaji wetu mkubwa ambao ni wafanyakazi wa benki ya NMB ambao bila wao, pengine tusingekuwa hapa tulisherehekea,” aliongeza.

Alibainisha kuwa benki yake kwa miaka mingi imekuwa na mchango mkubwa katika kusaidia shughuli mbalimbali za kiuchumi katika sekta nyingi ikiwemo Utalii, elimu, kilimo, miradi ya kimkakati ya muda mrefu na afya.

“Ninatoa tuzo hii kwa wadau wa benki ya NMB ambao wamejitolea kikamilifu katika azma yetu ya kubaki kweli bila kulinganishwa – benki imekuwa mstari wa mbele kwenye suala zima la ubunifu kwa kuzingatia wateja, uthabiti, uaminifu, usalama na usalama,” aliongeza.

Zaipuna mnamo Machi 2022 alitajwa kuwa miongoni mwa wanawake 74 wenye ushawishi mkubwa barani Afrika katika sherehe za wanawake wanaofanya biashara kubwa barani Afrika na data zilizotumika kutengeneza orodha hiyo ilitolewa kutoka Bloomberg kulingana na taarifa iliyotolewa na Africa.com.

Orodha hiyo iliwakilisha wanawake wanaofanya biashara kubwa barani Afrika. Biashara zote zinazoendeshwa na wanawake zenye Mapato ya Dola milioni 100 au zaidi.

Viongozi wengine wanawake waliotajwaa, ni pamoja Natascha Viljoen, Afisa Mkuu Mtendaji wa kampuni ya Anglo American Platinum; Nompumelelo Thembekile Madisa, Afisa Mkuu Mtendaji wa Bidvest Group na Leila Fourie, Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Johannesburg.

Viongozi wengine wanawake wa Afrika Mashariki kwenye orodha hiyo ni pamoja na Mitwa Ng’ambi, Afisa Mtendaji Mkuu wa MTN Rwanda Telecommunications, Kendi Ntwiga-Nderitu, Mwakilishi wa kampuni ya Microsoft nchi, Kenya na Brenda Mbathi, nktugugenzi wa kampuni ya General East Africa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles