27 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Cecafa yatibua ratiba Ligi Kuu

musonyeNa MWANDISHI WETU, DAR ES ALAAM

BARAZA la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), limethibitisha kuwa Kenya itakua mwenyeji ya michuano ya Kombe la Chalenji na michuano ya klabu bingwa (Kagame).

Michuano ya Chalenji imepangwa kufanyika Novemba mwaka huu, huku ile ya klabu imepangwa kufanyika Desemba ambayo ndiyo itaathiri Ligi Kuu Tanzania Bara.

Ligi Kuu Tanzania Bara Desemba inakua katika mzunguko wa pili, tofauti na Kenya wanakuwa katika mapumziko baada ya ligi kumalizika, hivyo kuondoka kwa Yanga kutaathiri ratiba.

Katibu wa Cecafa, Nicholaus Musonye, alinukuliwa na Mtandao wa Futaa akisema Kenya ambao ni wenyeji watawakilishwa na timu mbili za Gor Mahia na Ulinzi Stars.

“Tunafikiria kuwa na timu tatu, lakini nyingine itaingia baada ya kuona zile timu zilizoalikwa kama zitathibitisha ushiriki wao.

“Tunafikiria Kenya wataandaa mashindano mazuri kuliko yale yaliyowahi kufanyika,” alisema.

MTANZANIA lilimtafuta Katibu wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Celestine Mwesigwa, kujua kama wana taarifa hizo, ambapo alijibu hawakua na taarifa za mashindano hayo yote kufanyika Kenya.

“Niliongea na Musonye siku za karibuni, alichonieleza ni kuwa Chalenji itafanyika Sudan, hii ni taarifa mpya bado sijaipata,” alisema.

Kagame awali ilipangwa kufanyika Juni na Julai mwaka huu Zanzibar, baadaye mashindano hayo yalihamishwa ili yafanyike Tanzania Bara kutokana na Zanzibar ilikuwa imetoka katika uchaguzi, hivyo isingeweza kuwa mwenyeji lakini Bara napo yalishindikana baada ya TFF kusema hawakua wamejiandaa kuwa mwenyeji.

Hata hivyo, mashindano hayo yalishindikana kufanyika kwa muda uliopangwa baada ya kukosa nchi mwenyeji.

Mara ya mwisho Kenya kuwa mwenyeji wa Kagame ni mwaka 2001, ambapo Tusker ilikua mabingwa, pia nchi hiyo mara ya mwisho kuwa mwenyeji wa michuano ya Chalenji ni mwaka 2013 ambapo wenyeji hao walichukua kombe.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles