31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

CARDI B AMUOMBA RADHI BRUNO MARS

CALIFORNIA, MAREKANI

RAPA Belcalis Almanzar, maarufu kwa jina la Cardi B, amemuomba radhi msanii mwenzake Bruno Mars kwa kusitisha kuungana naye kwenye ziara yake ya muziki ijulikanayo kwa jina la 24K Magic Tour.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, mrembo huyo aliweka wazi sababu ya kushindwa kuungana kwenye ziara hiyo kuwa umri wa mwanaye ni mdogo.

“Nienza kwa kumuomba radhi Bruno Mars kuwa sitoweza kuungana naye kwenye ziara yake ya 24K Magic Tour ambayo inatarajia kuanza Septemba, nitashindwa kuungana naye kwa kuwa bado mwanangu ni mchanga sana, hivyo daktari wangu amenishauri nisifanye ziara yoyote ya muziki,” aliandika.

Hii ni wiki ya pili tangu mrembo huyo afanikiwe kupata mtoto wake wa kwanza na rapa mwenzake Offset kutoka kundi la Migos

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles