23 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 17, 2024

Contact us: [email protected]

Burundi yawatimua maofisa wa WHO

BUJUMBURA, BURUNDI

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) liko katika harakati za kuwahamisha wafanyakazi wake wanne kutoka nchini Burundi baada ya kuambiwa waondoke na Serikali.

Mkurugenzi wa kieneo barani Afrika, Dk Matshidiso Moeti, amethibitisha habari hiyo kwenye mkutano na waandishi wa habari, lakini akaongeza kuwa hajui ni kwanini viongozi walichukua hatua hiyo.

Hata hivyo Dk Moeti alisema kuwa licha ya kufukuzwa bado WHO itashirikiana na viongozi wa Burundi katika kukabiliana kwao na janga la virusi vya corona vinavyosababisha homa ya mapafu ikulikanayo kana Covid-19.

Hatua hiyo inajiri baada ya ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje nchini Burundi, uliotumwa mtandaoni kuwataka wawakilishi wa WHO kuondoka nchini humo ndani ya saa 48.

Dk. Walter Kazadi Mulombo ambaye alikuwa mwakilishi wa WHO nchini Burundi pamoja na wataalamu wengine Pr. Tarzy Daniel, Dk. Ruhana Mirindi Bisimwa na Dk. Jean Pierre Murunda Nkatawana wamepatiwa hadi Mei 15, 2020 kuondoka.

Katika mahojiano ya simu, Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Ezechiel Nibigira hakukataa wala kuthibitisha hatua hiyo.

Mfanyakazi wa wizara hiyohiyo alithibitishia BBC Idhaa ya Great Lakes uhalisia wa agizo hilo.

Sababu ya kufukuzwa kwa maofisa hao wa afya haikutajwa, licha ya juhudi za BBC kuzungumza na Walter Kazadi Mulombo.

Serikali ya Burundi inakabiliwa na ukosoaji mkubwa kwa kuandaa uchaguzi katika mazingira ya janga la corona, licha ya kuripoti kuwa na wagonjwa 27 na kifo cha mtu mmoja.

Kampeni ya wagombea urais zinafanyika kote nchini humo kabla ya uchaguzi utakaofanyika Jumatano, bila ya kuwa na utaratibu wa kukabiliana na maambukizi ya virus ya corona.

Hali hiyo imezua hofu ya kusambaa kwa virusi via ugonjwa wa Covd-19 katika taifa hilo dogo la Afrika Mashariki.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari kuhusi hali ya Burundi, siku ya Jumatano, Shirika la Kimataifa la kushughulikia hali ya dharura (International Crisis Group) lilisema Serikali ya Burundi halijakubali kuwepo kwa corona na kuongeza kuwa kutilia shaka idadi ya wagonjwa wa corona iliyotangazwa.

Mei 10, Serikali ya Burundi ilisema kwamba wachunguzi wote wa uchaguzi utakaofanyika Mei 20, 2020 watalazimika kufuata maagizo ya kukabiliana na virusi vya corona.

Hii ina maana kwamba wachunguzi wote ambao wanalenga kwenda katika taifa hilo ili kusimamia uchaguzi huo watalazimika kwenda karantini kwa siku 14 kuanzia siku watakapowasili nchini humo.

Na tangazo hilo lilitolewa wakati ikiwa ni siku 10 tu ndio zilizosalia kabla ya shughuli hiyo ya kidemokrasia kufanyika, hatua hiyo ilimaanisha kwamba wachunguzi kutoka mataifa ya kigeni hawataweza kuingia nchini humo.

Hatahivyo Jumuiya ya Afrika Mashariki ilisema kwamba italazimika kuwatumia maofisa wake waliopo nchini humo kusimamia shughuli hiyo.

Serikali ya Burundi imefunga mipaka yake ili kuzuwia kusambaa kwa virusi, na kuruhusu shehena za malori ya mizigo tu kuingizwa nchini kutoka mataifa jirani.

BBC

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles