30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Bunge kutofanya kazi na CAG, Mdee akalia kuti kavu kwa kumuunga mkono

Mwandishi Wetu, Dodoma

Bunge limeridhia kutofanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad, kutokana na kauli yake kuwa bunge ni dhaifu, hatua iliyolidhalilisha bunge.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Emmanuel Mwakasaka ametoa mapendekezo hayo bungeni leo Jumanne Aprili 2, wakati akisoma taarifa ya kamati hiyo iliyomhoji CAG kutokana na kauli yake hiyo ambapo ilimtia hatiani.

“Kamati ilimuuliza CAG Assad kama ataacha kulitumia neno dhaifu akasisitiza ataendelea kulitumia, hakuomba msamaha wala kujutia na akasisitiza ataendelea kulitumia neno hilo,” amesema Mwakasaka.

Aidha, baada ya kusoma taarifa hiyo, Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, aliwahoji wabunge kama wanakubaliana na mapendekezo hayo ambapo walikubaliana na uamuzi huo huku wengine wakipinga.

Katika hatua nyingine, kamati hiyo pia imependekeza Bunge kumsimamisha Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), kuhudhuria mikutano miwili ya Bunge kutokana na kuunga mkono kauli ya CAG.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles