31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Bobi Wine matatani tena

KAMPALA, Uganda

MBUNGE wa Jimbo la  Kyadondo Mashariki,  Robert Kyagulanyi, maarufu kama   Bobi Wine, amekamatwa tena  baada ya mashabiki wake kupambana na polisi wakipinga kufutwa matamasha  yake ya Pasaka yaliyokuwa yafanyike mjini hapa na katika miji ya  Arua na  Lira.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor, hali ya taharuki ilianza baada ya polisi kuzuia msafara uliokuwa ukiongozwa na mbunge huyo  kwenda katika ufukwe wa  One Love uliopo  eneo la Busabala.

Taarifa za gazeti hilo zilieleza kuwa baada ya Bobi Wine kukamatwa alitumbukizwa ndani ya gari la polisi na  kupelekwa mahali kusikojulikana .

Mashuhuda wa tukio hilo walieleza kuwa kabla ya ya mbunge huyo kukamatwa polisi wa kutuliza ghasia walivunja kioo cha gari lake  na kumvuta nje, lakini mwimbaji Nubian Li ambaye alikuwa naye hakukamatwa.

Mbali na mbunge huyo, waandaaji mashuhuri wa matamasha  ya muziki  Andrew Mukasa  na  Abbey Musinguzi maarufu kama  Abtex ambao waliandaa tamasha hilo la  Bobi Wine nao walikamatwa jana.

Taarifa zinaeleza kuwa wawili hao walikamatwa mapema  jana na kuzuiliwa katika gari moja la maofisa wa polisi kabla gari hilo kuondoka nao.

Kukamatwa kwa mbunge huyo ni baada ya Rais Yoweri Museveni kusema kuwa hatakubali matamasha ya muziki uliojaa siasa na kuonya kwamba katika siku zijazo hakuna mtu atakayefidiwa kwa matamasha ambayo yamefutiliwa mbali kutokana na siasa.

Rais huyo alitoa onyo hilo wakati wa mkutano na wanachama na waandaaji matamasha ya muziki nchini hapa na wamiliki wa maeneo ya kumbi za muziki katika Ikulu ambako alitoa Sh bilioni mbili za Uganda kama fidia ya hasara waliyopata baada ya maofisa wa polisi kufutilia mbali matamasha ya muziki wa Bobi Wine.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles