29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Bob Junior: Tutaonana baada ya uchaguzi

Bob JuniorNA THERESIA GASPER,

PRODYUZA na msanii wa Bongo Fleva, Raheem Rummy ‘Bob Junior’, amewataka mashabiki wake waonane baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 kwa kuwa sasa amebanwa na shughuli za uhamasishaji wa upigaji wa kura katika kampeni za wagombea urais.

“Sina mpango wa kuachia wimbo wala albamu yangu kwa sasa, lakini baada ya uchaguzi nitafanya hivyo kwa kuwa nitakuwa na muda mwingi wa kukaa studio na kuandaa muziki mzuri ambao kwa sasa sipati muda huo,” alisema

Bob Junior mkali wa wimbo wa ‘Nichumu’ anakuwa miongoni mwa wasanii wengine wengi wa muziki huo waliosimamisha shughuli zao za kimuziki kupisha shughuli za kisiasa ambapo wengi wao wameahidi kurudi upya na kutoa upya kazi zao za muziki baada ya Oktoba 25 uchaguzi utakapoisha na kutangazwa rais, wabunge na madiwani wa maeneo mbalimbali.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles