25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Blac avishwa pete ya uchumba

Blac Chyna Shops In The LA Fashion DistrictLAS VEGAS, MAREKANI

ALIYEKUWA mke wa msanii wa hip hop nchini Marekani, Tyga, Blac Chyna, amevishwa pete ya uchumba na kaka wa Kim Kardashian, Rob Kardashian.

Kupitia akaunti yake ya Instagram, Blac, mwenye umri wa miaka 27, ameweka picha yake huku akionesha pete hiyo ya dhahabu, huku picha nyingine ikimuonyesha akiwa na mpenzi huyo mpya.

Hata hivyo, Blac anaonekana kulipiza kisasi kutokana na baba mtoto wake, Tyga, kutoka na mdogo wake Kim, anayejulikana kwa jina la Kylie Jenner, hivyo Blac naye ameamua kutoka na kaka wa dada hao.

“Kitu chochote kinaweza kutokea hivi karibuni, naweza kusema kuwa nimempata mwanamume sahihi kwangu na yeye amepata mwanamke sahihi atakayedumu naye,” aliandika.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles