31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

BIASHARA Mtaji Soko la Hisa wapanda na kufikia bil 10/-

Patrick Mususa
Patrick Mususa

NA JOHANES RESPICHIUS, DAR ES SALAAM

MAMLAKA ya Masoko ya Mitaji (CMSA) imeidhinisha ongezeko la ukubwa wa mtaji wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) kutoka Sh bilioni 8.25 hadi Sh bilioni 10.12.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Meneja Mauzo DSE, Patricki Mususa, alisema kutokana na kuvuka lengo la mauzo ya awali ya IPO ya hisa zake la kufikisha Sh bilioni 7.0, DSE imefanikiwa kukusanya Sh. bilioni 35.768 sawa na asilimia 377.

“Mei 16, mwaka huu, DSE iliendesha mauzo ya IPO ya hisa zake ikiwa na matarajio ya kukusanya mtaji wa Sh  bilioni 7.5 kutokana na mauzo ya hisa bilioni 15 kila moja kwa Sh  500, kufuatia mauzo hayo DSE imefanikiwa kukusaya mtaji wa bilioni 35.768 sawa na  ongezeko la asilimia 377.

“Utaratibu wa ugawaji wa hisa utakuwa hivi, waombaji wa hisa zenye thamani ya Sh  milioni 5 watapatiwa zote lakini wale ambao ni zaidi ya hapo watapata hisa sawa na mgawanyo unaoendana na ukubwa wa maombi na pia watarudishiwa fedha zao kulingana na kiwango cha ugawaji,” alisema Mususa.

Aidha alisema wafanyakazi wa DSE watapata asilimia 3 ya hisa na kwamba fedha zitakazorudishwa zitakuwa kwa utaratibu wa hundi pamoja na usajili wa akaunti za CSD utakaokamilika Julai 11, mwaka huu.

Katika hatua  mwingine, Mususa alisema kuwa idadi ya mauzo katika soko hilo imeshuka kwa asilimia 77 kutoka Sh bilioni 29.1 wiki iliyopita hadi Sh bilioni 6.6 wiki hii huku idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa ikipanda kwa asilimia 113 kutoka milioni 2.5 hadi milioni 5.4

Sambamba na hilo alisema ukubwa wa mtaji wa soko umeshuka kwa asilimia 0.6 kutoka Sh trilioni 21.0  hadi Sh trilioni 21.7, wakati mtaji wa makampuni ya ndani ukishuka kwa asilimia 0.9 hadi kufikia trilioni 7.9.

Alisema makampuni matatu yaliyoongoza kwa idadi ya hisa zilizonunuliwa na zilizouzwa ni Benk ya CRDB asilimia  66.87, NMB asilimia 18.64 na kampuni ya bia TOL asilimia 8.72.

“Kiashiria cha sekta ya huduma za kibenki na za kifedha kimeshuka kwa pointi 86.46 kikiwa kimechangiwa na kupanda kwa bei ya hisa kwenye kaunta za NMB (1.79%) na CRDB (6.25%),” alisema Mususa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles