26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Bei ya Petroli yazidi kushuka

FELIX NGAMLAGOS.MKURUGENZI EWURA TZNa Maneno Selanyika, Dar es Salaam

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza kushuka kwa bei ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa, ikilinganishwa na bei ya mwaka jana.

Taarifa iliyotolewa na EWURA jana na kusainiwa na Mkurugenzi Mkuu wake, Felix Ngamlagosi, ilieleza kuwa bei hiyo elekezi itaanza kutumika kuanzia leo Januari 6.

Ngamlagosi alitaja sababu mojawapo ya kupungua kwa bei za mafuta ni kushuka kwa  bei za mafuta katika soko la dunia, pamoja na kushuka kwa gharama za usafarishaji na uletaji wa bidhaa hizo.

“Bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya aina hizo, zimeshuka ikilinganishwa na toleo lililopita la Desemba 2 mwaka jana ambapo kwa mwezi huu  bei za rejareja kwa mafuta hayo zitapungua kama ifuatavyo Petroli Lita 79 itapungua kwa asilimia 4.01, Dizeli lita 76 punguzo ni asilimia 4.20 na Mafuta ya taa lita 66 itakuwa asilimia 3.73,” ilisema taarifa hiyo.

Katika taarifa hiyo, mamlaka hiyo imewataka wananchi kuzingatia mambo muhimu ambayo ni pamoja na kulinganisha bei hizo za mafuta na zile za toleo la Desemba mwaka jana ambazo zilikuwa Petroli Sh 79.19 kwa lita sawa na asilimia 4.23, Dizeli Sh 76.49 kwa lita sawa na asilimia 4.45 na Mafuta ya Taa Sh 65.86 kwa lita sawa na asilimia 3.97, Alisema kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2008, bei za bidhaa hizo zitaendelea kupangwa na soko.

 

“EWURA itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta. Taarifa hizi zina lengo la kuwasaidia wadau kufanya maamuzi stahiki kuhusu manunuzi ya bidhaa za mafuta.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles