30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Batuli: Watoto wangu sitaki wawe waigizaji

Yobnesh Yusuph ‘Batuli’
Yobnesh Yusuph ‘Batuli’

NA BEATRICE KAIZA,

MKALI wa filamu nchini, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’, amesema hataki watoto wake wawe waigizaji kwa kuwa kuna mambo mengi anayokutana nayo na hataki wakutane nayo.

Akizungumza na MTANZANIA, Batuli alisema hataki watoto wake, Samir na Malima, wawe waigizaji kwa kuwa amekutana na mambo mengi mabaya yakiwemo kutukanwa mitandaoni, kupandishiwa bei za vitu kiasi kwamba vinasababisha wakati mwingine aishi maisha ya kuigiza.

“Wasanii wengi Tanzania wanaishi maisha ya kuigiza hivyo sitaki watoto wangu waishi katika sanaa kwa sababu wanaweza kuishi kwa kuigiza, nataka wafanye shughuli nyingine nitawasaidia wafikie malengo yao kupitia elimu,” alisema Batuli.

Batuli aliongeza kwamba urithi pekee anaotaka kuwaachia watoto wake ni mali na elimu huku akiwahasa watoto nchini wasome kwa bidii kwa kuwa elimu ndiyo kila kitu katika maisha.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles