Rais wa Gambia, Adama Barrow, anatarajiwa kurudi nyumbani rasmi leo jioni kuchukua nafasi yake ya uongozi.
Kwa mujibu wa Wanadiplomasia, wamemtaka Barrow arudi mara moja nyumbani kuepuka pengo la uongozi.
Taarifa zinasema Barrow atakaa katika makaazi yake wakati ukaguzi ukifanywa katika ikulu kutambua hatari yoyote kufuatia kuondoka kwa Yahya Jammeh kwenda uhamishoni Guinea ya Ikweta.
Bado baadhi ya wanajeshi wa mataifa ya Afrika magharibi wapo Gambia wakiendelea kuimarisha hali ya usalam nchini humo.
Barrow aliapishwa wiki iliyopita nchini Senegal kutokana na kugoma kujiuzulu kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Yahya Jammeh.