28.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Barnaba afichua siri ya mifuko yake kutuna

Barnaba akitumbuizaNA THERESIA GASPER

MSANII wa Bongo Fleva, Elias Barnabas ‘Barnaba Boy’, ametoa siri ya mifuko yake kutuna pindi anapokuwa jukwaani akifanya shoo.

Barnaba aliweka wazi siri hiyo hivi karibuni alipotembelea Ofisi za New Habari (2006) Ltd zilizopo Sinza jijini Dar es Salaam zinazochapisha magazeti ya Mtanzania, Bingwa, Dimba, Rai na The African.

Alisema mifuko yake hutuna kwa kuwa huweka waleti zilizojaa fedha kwenye mifuko ya mbele huku akiongeza kwamba pia hiyo ni alama yake ya kumtofautisha na wasanii wengine pindi awapo jukwaani.

“Hii si kwangu tu ila inatokea kwa baadhi ya wasanii unakuta wengine wameweka vitambaa vya kufutia jasho, ila mimi huwa naweka fedha nikimaanisha nipo kazini na ndiyo mwonekano wangu,” alieleza Barnaba.

Barnaba alisema kila msanii anakuwa na staili yake ili tu kuwapa ladha yenye utofauti mashabiki wake na kuwa na utofauti na watu wengine.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles