27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

BancABC kuchochea uchumi tegemezi kwa watu wenye ulemavu nchini

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Banki ya BancABC imeahidi kuendelea kushirikiana na serikali katika kuhakikisha kuwa inawawezesha watu wenye ulemavu kuweza kufikia malengo yao ya kiuchumi na kielimu.

Hayo yameelezwa juzi jijini Dodoma na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya ABC, Imani John Bgoya, wakati wa kongamano la kuwajengea uwezo wa uchumi tegemezi watu wenye ulemavu lililofanyika jijini.

Baadhi ya watendaji wa Benki ya ABC wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa Mkutano Mkuu wa Uchumi na Mapendekezo ya Siku ya Mwanamke Mwenye Ulemavu Tanzania uliofanyika jijini Dodoma, jana.

Moja ya taasisi zilizoshiriki kongamano hilo ambalo mgeni rasmi alikuwa Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson, ni pamoja na Ikupa Trust Fund.

“Sisi BancABC tunayo furaha kubwa kuungana na Ikupa Trust Fund kuwawezesha watu wenye ulemavu kupata haki ya elimu, maarifa pamoja na ujuzi kwa kuwajengea uwezo wa kufikia mafanikio yao na familia zao ili wamudu kujikimu kimaisha wakati wowote.

“Uamuzi wa serikali kurekebisha sheria ya fedha ya LGA ya kutenga asilimia 10 kwa ajili ya Wanawake na Vijana na sasa kuwajumuisha watu wenye ulemavu ni moja ya sababu kubwa inayodhihirisha kwamba kundi linapaswa kupewa kipaumbele sio tu na serikali bali pia na jamii kwa ujumla na ndio sababu sisi BancABC, pia tumeunganisha nguvu na Ikupa Trust Fund ili kuweza kufanikisha kongamano hili la siku mbili ili mafanikio yake yaweze kuleta suluhisho la kifedha kwa watu wenye ulemavu,” amesema Bgoya.

Amesema BancABC kwa kushirikiana na serikali imejizatiti kuendeleza suluhisho la kifedha kwa kutanua wigo wa huduma za kifedha na kuzileta karibu na wananchi wa Tanzania kwa nia ya kupunguza idadi ya wananchi ambao hawajafikiwa na huduma za kifedha na kusaidia kuinua maisha ya wananchi kwa kuongeza upatikanaji wa huduma hapa nchini.

“Nikudhihirishie kwamba kwa hayo yote BancABC imedhamiria kuendelea kuunga mkono watu wanaoishi na ulemavu kwa sababu afya na ulemavu ni moja ya lengo letu Kubwa la kuweza kurundisha kwa jamii.

“Mwaka 2018 tulishirikiana na Ikupa Trust Fund kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani – kupitia tukio hilo la kila mwaka lenye lengo la kuongeza uelewa kwa watu wenye ulemavu – kukuza maendeleo yenye ujumuishi na watu wenye ulemavu kwenye jamii. Sisi bado tutaendelea kuja na ubunifu zaidi wa mbinu tofauti tofauti ili kukuza ushirikiano huu zaidi na kufanya kazi sambamba na malengo ya serikali kwa lengo la kuendelea kuleta suluhisho la huduma za kifedha kwa makundi yote hapa nchini,” amesema Bgoya.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Angelina Mabula akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya ABC, Imani John Bgoya pamoja na Watendaji wa benki hiyo mara baada ya Mkutano Mkuu wa Uchumi na Mapendekezo ya Siku ya Mwanamke Mwenye Ulemavu Tanzania uliofanyika jijini Dodoma, jana.

Ameongeza kuwa: “Mwaka 2018, BancABC ilizindua tawi lake hapa Dodoma kwa lengo hilo hilo, Pia hadi sasa tunazo ofisi 10 ndogo za mauzo ambazo zinatoa huduma ya mikopo kwa wafanyakazi wa serikali kwa mkoa huu wa Dodoma. Pia tuko kwenye mazungumzo na wadau ili kuja na pendekezo la dhamana kwa huduma za kifedha kwa watu wenye ulemavu hapa nchini.

“Lengo ni kuongeza chachu kwa Watanzania kujua na kuwa na utamaduni wa kuweka akiba, kupata riba na kisha kukopa, tumeweza kuzindua huduma ambazo zinawafanya wateja wetu kupata riba kutoka kianzio cha chini cha Sh 10,000 na kisha baadae kukopa kulingana na amana yake na hivyo kuweza kuwawezesha wateja wetu kifedha,” amesema Bgoya.

Ameongeza kuwa benki hiyo itaedelea kuongeza suluhisho katika sekta ya huduma za kifedha kupitia huduma zake mbalimbali inazotoa kwa wateja wake nchini wa soko la kawaida na hata wale wa makampuni tanzu kupitia kwenye matawi yake yote.

“Tuna mawakala wetu zaidi ya 300 pamoja na ofisi zetu ndogo za mauzo zaidi ya 100 zilizoenea kote nchini. Kwa kupitia njia hii tumefanikiwa kusambaza huduma, na kuwafikia Watanzania walio wengi. Kupitia BancABC Mobi USSD na applikesheni, huduma za benki kwa njia ya mtandao ambazo zinawawezesha wateja wetu kupata huduma za kutoa fedha, kuweka na kupata riba wakiwa popote pale.

“Vile vile tunazo kadi za malipo ya kabla ambazo zinapatikana kwenye sarafu 6 ambazo zinawawezesha wateja kufanya malipo bure kwa njia ya mtandao na kwenye vituo vya malipo yaani POS. Vile vile wanaweza kutoa fedha kwenye mashine za ATM za VISA wakati wowote na popote duniani,” amesema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles