24.7 C
Dar es Salaam
Tuesday, March 19, 2024

Contact us: [email protected]

‘Bam Bam’ ya Jdart, Madematrix gumzo

NA CHRISTOPHER MSEKENA

MSANII wa kizazi kipya kutoka Japan, Jdart, amewaweka tayari mashabiki kwa ujio wake mpya kupitia kolabo, Bam Bam aliyofanya na mwanamuziki wa Kitanzania, Madematrix itakayotoka hivi karibuni.

Akizungumza na MTANZANIA, Jdart mwenye asili ya Jamaica alisema msimu huu ni msimu wa burudani kwahiyo ameamua kuja na kolabo hiyo yenye muziki wa kuchezeka uliofanyika chini ya prodyuza wa Kitanzania, Fraga.

“Tunaelekea msimu wa sikukuu, natamani hii Bam Bam ikawabambe huko kwenye maklabu wanapokula bata, ngoma itatoka muda wowote kutoka sasa ila tangu nimeachia ‘cover’ ya ngoma, ‘cover’ imekuwa gumzo kwahiyo unaweza kuona ni jinsi gani mashabiki wanaisubiri,” alitamba Jdart.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
584,000SubscribersSubscribe

Latest Articles