23.1 C
Dar es Salaam
Sunday, September 8, 2024

Contact us: [email protected]

Balozi awapa mzuka Simba kuimaliza Platinums

Na Winfrida Mtoi

Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Profesa Emmanuel Mbennah, amekiongezea mzuka kikosi cha Simba baada ya kuwataka wachezaji waondoe hofu na kufanya kama walichowafanyia Plateau United ya Nigeria.

Balozi ametoa kauli hiyo leo alipokutana na wachezaji wa Simba, walipowasili Zimbabwe kujiandaa na mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya FC Platinums ya nchini huko utakaochezwa Jumatano ya wiki ijayo.

Balozi Mbennah, amewapongeza wachezaji wa Simba na kusema timu ya waliyokutana nayo awali ya Plateau United haikuwa ya kinyonge, lakini waliweza kuiwakilisha Tanzania.

“Mnacheza vizuri sisi tunawatazama katika runinga mliifunga ile timu ya Nigeria, tunafikiri mtaendelea vizuri kwa sababu hatuna wasiwasi, nadhani kuna Watanzania wengi hapa na sisi tutakuwepo pamoja nanyi,” amesema Balozi Mbennah.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles