31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Baba aishi kinyumba na mtoto wake miaka mitatu

2963597502_755fac524f_b

Mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Tambukareli wilayani Nyamagana  mkoani Mwanza  (jina linahifadhiwa) anadaiwa kubakwa na kulazimishwa kuishi kinyumba na  baba yake mzazi Paul  Jonas (43) kwa muda wa miaka mitatu.

Mtoto huyo mwenye umri wa miaka 10 sasa inadaiwa alianza kuishi kinyumba na baba yake huyo tangu akiwa na miaka nane.

Kwasasa anatembea kwa shida sana kutokana na  maumivu aliyoyapata kutokana na ukatili wa baba yake mzazi.

Alisema wakati baba yake alipoanza mchezo huo alikuwa akimtishia kuwa endapo atajaribu kumwambia mtu yeyote kuhusu mchezo huo atamchinja na kukimbia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na mtuhumiwa huyo anashikiliwa na jeshi la polisi.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles